Pages

Thursday, April 27, 2017

Fahamu: Samaki zebra anayetibu uti wa mgongo.

Watafiti kutoka Marekani wamebaini aina ya samaki aitwae Zebra Fish, ambaye anaweza kuzalisha upya, uti wake wa mgongo wa mwanadamu unapovunjika.
Watafiti hao wamesema kuwa samaki huyo ana uwezo wa kulizalisha upya uti wa mgongo unapovunjika kwa kuziunganisha kama daraja, sehemu zilizokatika kwa kutumia aina ya protini mwilini mwa samaki huyo.
Binadamu anayo aina hiyo ya protini inayoweza kuzalisha mifupa, lakini haifanyi kazi sawa na ile ya samaki Zebra. Aina hiyo ya protini kwenye binadamu inafanana kwa asilimia 90 na aina hiyo kwenye samaki hao.

Kuwepo kwa mpango wa chanjo kwa umma dhidi ya homa ya uti wa mgongo barani Afrika umepata mafanikio makubwa. Zaidi ya watu milioni mbili wamepata kinga dhidi ya maradhi hayo, kutoka nchi zipatazo 16 barani Afrika, kutoka Gambia mpaka Ethiopia.
Shirika la Afya Duniani limesema katika kipindi cha mwaka 2013, kulikuwa na wagonjwa wanne tu, katika bara hilo ambalo awali, liliweka rekodi ya kuwa na maelfu ya vifo vinavyotokana na ugonjwa huo wa homa ya uti wa mgongo. Kila mwaka, kampeni ya kupambana na ugonjwa huo ilianza mwaka 2010.
wepo wa samaki zebra atasaidia kupunguza ama kuondoa ugonjwa huo duniani kote.

No comments:

Post a Comment