Advertise with us here... Contact: 0654 264 472 Email: sabanhussein@yahoo.com sabanhussein@yahoo.com

Monday, October 31, 2016

Ni muda mrefu sijaonana na Ray C wala hatuongei ila namuombea – Lord Eyes





Rapa huyo mwenye makazi yake mkoani Arusha, amesema anamuombea mwanadada huyo kwani kwa matatizo aliyonayo ni kama maradhi hivyo hayaponi kwa siku moja.
“Sijakutana naye wala hatuongei ila namuombea Mungu kwani tatizo lile ni kama maradhi mengine hivyo haliwezi kuisha kwa mara moja linachukua muda, anahitaji maombezi na mimi namuombea kama navyojiombea mimi nifanye kazi zikamilike tukutane kwenye show huko” Lord Eyez alikiambia kipindi cha Enewz cha Eatv.
Pia Lord Eyez amesema bado anaona Ray C ana nafasi ya kufanya vizuri kwenye muziki kwa kuwa hakuna msanii kwenye muziki anayefanya muziki wa aina yake.
“Leo hii kwenye muziki hatumuoni mtu kama Ray C, mpaka sasa hakuna mtu kama Ray C hivyo chumba chake kwenye muziki bado kipo kinamsubiri arudi tu,” alisema Lord Eyez.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

273511

Popular Posts

Unordered List

http://michuzijr.blogspot.com/2013/03/party-kubwa-ya-pasaka-kudondoshwa.html

Flickr Images

Follow Us

Bin Hussein65 copyright 2014. Powered by Blogger.

Translate

Followers

Search This Blog