Advertise with us here... Contact: 0654 264 472 Email: sabanhussein@yahoo.com sabanhussein@yahoo.com

Thursday, October 27, 2016

Jay Z ajipanga kutoa $40m kununua nyimbo za Prince

Bosi wa mtandao wa Tidal, Jay Z ameanza kujaribu kupata haki miliki ya nyimbo za marehemu Prince aliyefariki mwezi April, mwaka huu.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, Jay Z alikutana na mmoja wa ndugu wa Prince, Tyka na kumueleza kuwa yupo tayari kununua haki miliki za nyimbo za Prince ambazo bado hazijatoka kwa kulipa kiasi cha dola milioni 40.
Hata hivyo Tyka hana haki ya kusaini mkataba huo mpaka pale atakapokutana na meneja wa marehemu Prince na baadhi ya ndugu zake wengine wenye haki na nyimbo hizo. Kabla ya kifo chake, Prince aliwahi kuachia nyimbo zake kwenye mtandao wa Tidal lakini pia wawili hao walikuwa na urafiki wa ukaribu.
Jay Z aliwahi kurap kwenye wimbo wa ‘All The Way Up (Remix)’, “Prince left his masters where they safe and sound. We never gonna let the elevator take us down.”

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

273594

Popular Posts

Unordered List

http://michuzijr.blogspot.com/2013/03/party-kubwa-ya-pasaka-kudondoshwa.html

Flickr Images

Follow Us

Bin Hussein65 copyright 2014. Powered by Blogger.

Translate

Followers

Search This Blog