Advertise with us here... Contact: 0654 264 472 Email: sabanhussein@yahoo.com sabanhussein@yahoo.com

Thursday, October 27, 2016

Ndoa ya Tundaman yamtamanisha Dogo Janja naye kuvuta jiko

Usishangae pale utakapopokea ujumbe wa Dogo Janja akikuomba mchango wa harusi (iwapo atafanya hivyo). Ni kwasababu muimbaji huyo wa Kidebe anaweza kuwa ameshawishika kujiunga na kambi ya wavaa pete kwenye kidole cha chanda – asante kwa ushawishi alioupata kutoka kwa Tundaman.

Tunda aliuaga ukapera wiki iliyopita katika harusi iliyofanyika huko Morogoro na mchakato mzima ulimshawishi Janjaro kufikiria kufanya kitu kama hicho.
Akiongea na Clouds TV, Madee alidai kuwa Janjaro alikuwa Moro kwa takriban wiki nzima katika maandalizi ya harusi hiyo na amejifunza mengi.
Madee amesema kuna vitu vingine huenda Dogo Janja amevitamani kupitia harusi hiyo. Hata hivyo amedai kuwa hana uhakika iwapo kijana wake huyo alimaanisha kweli au aliropoka tu.

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Total Pageviews

273618

Popular Posts

Unordered List

http://michuzijr.blogspot.com/2013/03/party-kubwa-ya-pasaka-kudondoshwa.html

Flickr Images

Follow Us

Bin Hussein65 copyright 2014. Powered by Blogger.

Translate

Followers

Search This Blog