Navy Kenzo wasema lengo lao kwa sasa ni kwenda Billboard na Grammy
Kundi la Nany Kenzo limekuwa nominated kwenye tuzo za MTV Africa Music Awards ambazo zitafanyika Afrika Kusini Octoba 22 mwaka huu.
Akiongea katika kipindi cha The Playlist cha Times FM Jumamosi hii, Navy Kenzo wamesema tayari kwa sasa wanakolabo za kutosha na wasanii wa Afrika ambazo zitawatangaza vizuri Afrika.
“Tutegemee kolabo zaidi na wasanii wakubwa duniani, ndoto yetu mwaka huu ni kwenda Billboard, kwenda Grammy na kufanya vitu vikubwa zaidi, kwa hiyo tunashukuru Mungu connetion zinazidi kuwa kubwa,” alisema Aika.
Kundi hilo mpaka sasa lina kolabo na Patoranking pamoja na Bana Boy wa Nigeria ambazo hazijatoka mpaka sasa
0 comments:
Post a Comment